Haya sasa 50 Cent ndani ya Bongo!!
Wiki iliyopita tuliandika juu ya ujio wa wasanii maarufu duniani wa kundi la G-Unit nchini Afrika Kusini ambapo zilizuka hoja nyingi zilizokuwa zimedai kuwa ujio huo kwa Tanzania bado ni ndoto…
Wiki iliyopita tuliandika juu ya ujio wa wasanii maarufu duniani wa kundi la G-Unit nchini Afrika Kusini ambapo zilizuka hoja nyingi zilizokuwa zimedai kuwa ujio huo kwa Tanzania bado ni ndoto.
Sasa Bongo5 inakuhabarisha kuhusiana na ujio wa 50 Cent ambaye anatarajiwa kushuka mwezi ujao kwa ajili ya kufanya makamuzi ya kufa mtu!! Hapo vipi?
Msanii maarufu na kiongozi wa kundi la G-Unit anatarajiwa kushuka nchini kwa ajili ya kufanya onesho moja ambalo limedhaminiwa na kampuni kuubwa ya mawasiliani Tanzania Tigo ambayo imekuwa ikikamua ile mbaya katika pande wa burudani hapa nchini.
Siku chache zimepita tangu kampuni hiyo iwalete wasanii toka nchini Marekani KC n Jojo na safari hii wanakuja na mtu mzima Curtis Jackson a.k.a 50 Cent; hatujui baada ya hapo watamleta nani, pengine waweza kusikia Diddy, R-Kelly au Ciara