Bongo Movie
Kelvin aibiwa
(Kelvin aliyevaa kofia akiwa na Zola D siku ya pambano ambalo Zola ilibidi apambane na Kiza kinene) Msanii aliyewahi kufanya vizuri kwenye filamu na maigizo Tanzania Kelvin, amewalalamikia wasanii wenzake kwa vitendo vya ubaguzi.
Nyota huyo alisema amesaidia wasanii wengi kutoka kupitia mgongo wake lakini sasa wanamdharau.
Alisema hayo baada ya msanii mmoja maarufu kuigiza filamu yake, lakini baadaye kumzungusha katika kupiga picha ya Kava.
“Wasanii tunakuwa hatukumbuki wapi tulipotoka, hivyo tunajisahau haraka na kukosa ushirikiano” alisema.
Hivi karibuni msanii huyo, aliibiwa video Production, filamu zilizokamilika saba na kompyuta na fundi aliyekuja kutengeneza kompyuta hiyo.