Bongo Movie
Mapigo matatu
Kundi la maigizo la Louches, linatarajia kuachia filamu yao mpya itakayo kwenda kwa jina la Mapigo matatu, ambayo itafanywa chini ya Kampuni ya Louches iliyopo Kawe . Akiongea kiongozi wa kundi hilo anasema filamu yao itakuwa inazungumzia maisha ya kawaida ya mtanzania,
ambao miongoni mwao wanajikuta wakiacha shule na kutumbukia kwenye vitendo viovu kama ujambazi na umalaya ambao unapelekea vifo vyao, filamu hiyo pia imekusanya wasanii wachanga na wale ambao tayari wameshaanza kuwa na jina kama Riyama na Mzee Magari.