Burudani

Mimi ni mkali wa kuvaa zaidi ya Dogo Janja – Harmorapa

Mkali wa wimbo ‘Kiboko ya Mabishoo’ Harmorapa amemtaka Dogo Janja kuacha kujinadi kuwa yeye ni mkali wa kuvaa.

Harmorapa

Rapa huyo ambaye wiki hii ameachia wimbo wake mpya ‘Nundu’ , amedai yeye ni mkali wa kuvaa kuliko hata mkali huyo  wa ‘Kidebe’ kutoka Tip Top Connection.

“Dogo Janja asijinadi sana kwenye kuvaa, mwambie tupo wanyamwezi kama sisi tunavaa pamba kali,” alisema Harmorapa.

Aliongeza, “ Najua na yeye ni mkali wa kuvaa lakini mimi ni mkali zaidi kwenye hizo, kwanza angalia jinsi nilivyotupia leo, kinyamwezi,”

Katika hatua nyingine rapa huyo amesema anamkubali sana Dogo Janja kwa kuwa ni msanii kijana ambaye amejaribu kufanya mambo makubwa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents