Michezo
Mwanariadha wa kike wa Afrika Kusini, Caster Semenya apata jiko!
Mwanariadha controversial wa nchini Afrika Kusini, Caster Semenya amedaiwa kufunga ndoa.
Taarifa zimedai kuwa Semenya alifunga ndoa ya kimila wikiendi iliyopita.
Caster na mpenzi wake wa muda mrefu Violet Raseboya walisherehekea harusi yao huko Ga-Dikgale kwenye wilaya ya Capricorn ya Limpopo.
Hata hivyo ndugu zake wa karibu wamekanusha taarifa hizo huku wengine wakidai huenda ilikuwa ni sherehe ya kuchumbiana tu.