Bongo Movie
Mzee Magari ajiita Mzee wa Masauti
Baada ya kuibuka majina mengi kama Vijana wa Masauti, mwalimu wa Masauti, rais wa masauti lakini sasa, msanii wa filamu Tanzania Charles Magari maarufu kama mzee Magari amesema yeye kwa sasa anatambulika kama Mzee wa Masauti, pia ameazisha kampuni yake ya filamu inayoitwa Masauti Sample Film ikifanya kazi ya kuedit na kushoot Movie.
Mwigizaji huyo anatumia jina hilo hasa kutokana na sauti jinsi ilivyokuwa nzito na kuweza kuitumia kisanii zsaidi kiasi na kuleta mvuto wa aina yake. Anasema kwa sasa analengo la kutoa vipaji vipya kwenye filamu kupitia kampuni yake ya Masauti.