Habari
Orijino Komedi leo kusaini deal mpya ya usimamizi + picha ya ghorofa jipya la Masanja
Kundi la wachekeshaji wa kundi la Orijino Komedi leo linasainia mkataba mpya wa menejimenti. Muda huu waigizaji wa kundi hilo wapo Serena Hotel jijini Dar es Salaam kuzungumza na waandishi wa habari.
Waandishi wa habari wakiwa kwenye hoteli ya Serena ambapo OK watasaini mkataba na management mpya
Picha za tukio hilo tutakuletea baadaye.
Wakati huo huo, Masanja Mkandamizaji ameonesha picha ya nyumba yake mpya ya ghorofa moja iliyopo jijini Dar es Salaam. Masanja ameionesha picha hiyo kupitia Instagrama na kuandika: Glory be to God.
Licha ya kupata fedha kutokana na kazi zao za usanii, wasanii wengi wa Orijino Komedi akiwemo Masanja ni wakulima wazuri.
Masanja akiwavuna mpunga aliolima huko Mbarali