Habari

Rais Magufuli amteua Bi. Mwanana Msumi kuwa Katibu Tawala (DAS) Kisarawe

Baada ya kutengua uteuzi wa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kisarawe, Mtela Mwampamba, Rais Magufuli amemteua Bi. Mwanana Msumi ambaye alikuwa Afisa Tawala kushika nafasi hiyo kuanzia leo Juni 28, 2020.

Bi. Mwanana Msumi anachukua nafasi ya Katibu Tawala (DAS) wa Wilaya ya Kisarawe Mtela Mwampamba, kwa madai ya kwamba amekuwa akifanya mambo ambayo hayaendani na maadili ya kazi yake ikiwemo tuhuma za kuchukua wake za watu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents