Habari

Samsung yaipiga kikumbo Apple kwa kutajwa kama kampuni ya ‘Smartphone’ inayouza zaidi duniani

Kampuni ya Samsung imeweka record nyingine baada ya kumpita mpinzani wake Apple kwa kutajwa kuwa kampuni ya simu za mikononi ‘smart phone’ inayotengeneza faida kubwa zaidi duniani kwa sasa.

samsung-galaxy-s4-black-white

Kwa mujibu wa wachambuzi wa sekta hiyo Kampuni ya Apple imejikuta ikiporomoka sokoni kwa 14% katika kipindi cha miaka mitatu kutokana na kutofanya vizuri katika toleo lake la iPhone 5 pomoja na ushindani mkubwa kutoka kwa wapinzani hasa Samsung.

Samsung kampuni ya Kikorea inakadiriwa kutengeneza faida inayofikia £3.4billion kupitia simu zake za mkononi za Android katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka huu na kutengeneza asilimia 27.7 ya simu zote za mkononi zilizouzwa sokoni mwaka huu.

iphone5

Wachambuzi wameendelea kusema mauzo ya simu aina ya iphone zinazotengenezwa na Apple yamekuwa chini ya kiwango kwa £3billion kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Strategy Analytics.

Simu za iphone zimeendelea kupata upinzani mkubwa kutoka kwa Samsung hasa baada ya kampuni hiyo ya kikorea kutambulisha Galaxy S4 iliyochangia Samsung kufanya vizuri zaidi sokoni kwa kipindi cha karibuni.

Hata hivyo wataalam wanasema Apple inauwezo wa kuipita tena Samsung endapo watazindua toleo lijalo la iphone.

SOURCE: DAILY MAIL

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents