Michezo
Antonio Nugaz na kauli ya kishujaa: MO Simba Bunju Arena pale pale tupo tayari kucheza (+Video)
Afisa Mhamasishaji na Msemaji wa Klabu ya Yanga SC, Antonio Nugaz amesema baada ya ushindi wao wa jana dhidi ya Gwambina FC wapo tayari kucheza na timu yoyote na yoyote, mahala popote na hata Wakitaka huko Mo Simba Bunju Arena akionekana kama akitupa jiwe gizani kwa watani wao wa jadi Simba. Katika kusisitiza hilo Nugaz amesema mchezo wao dhidi ya Azam FC itakuwa ni salamu tosha.