Burudani
Afande Sele kuja na albam mpya ‘Kingdom ya Amani na Upendo’
Rapper Mkongwe kutoka Morogoro, Seleman Msindi aka Afande Sele aliyekaa kimya kwa muda pasipo kutoa albam, amesema anatarajia kuuvunja ukimya huo kwa kuachia albam mpya Kingdom ya Amani na Upendo.
Hata hivyo Afande amesema licha ya soko la mauzo ya albam kusuasua hatojali mauzo mabaya kwakuwa lengo lake ni kuielimisha jamii na sio kupata maslahi kutokana na mauzo ya albam hiyo.
“Sitofikiria soko kama litalipa au vipi ninachohitaji ni kuwapa elimu Watanzania,” amesema Afande. Pia ameongeza kuwa mashabiki wataweza kuinunua albam hiyo kwa njia ya simu.