Alikiba alininunulia viatu vya mpira – Ricardo Momo kaka yake na Diamond
Kaka yake na diamond Ricardo Momo amezungumza na @el_mando_tz na kuzungumza menngi kuhusu maisha yake nje ya Wasafi Media akiwa kama mchambuzi.
@el_mando_tz amemuuliza kuhusu ukaribu wake na Alikiba maana wote wamezaliwa na kukulia Kariakoo ingawa mitaa ni tofauti.
Ricardo amesema kuwa ni kweli wamekulia wote Karikaoo na Alikiba na zamani walikuwa waenda kucheza PS nyumani kwa Alikiba hasa mdogo wake Idd Santos.
Ameongeza kuwa ukaribu ulipungua baada ya migogoro ya Diamond na Alikiba licha ya kuwa mdogo wake alikuwa bado na ukaribu ila sio kama zamani.
Amekumbushia kuwa siku moja Alikiba alimnunulia Ricardo Momo viatu vya mpira, sikuwa na hela nikamuomba akanipa elfu 20 nikaenda Karume kununua viatu vya mpira vipya.
Inertview nzima ipo katika akaunti yetu ya Youtube ya Bongofive.