Habari
Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu akamatwa na watu wasiojulikana
Aliyekua Mbunge wa Singida Kaskazini na Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu amekamatwa na kuchukuliwa na watu wasiojulikana akiwa katika kikao cha ndani cha Chadema kwenye kata ya Itaja, wilaya ya Singida vijijini mkoani Singida.
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na CHADEMA zinaeleza kuwa, Nyalandu amekamatwa na watu wanaodhaniwa ni TAKUKURU na kwasasa yupo Singida Mjini.
Hta hivyo Chadema wamesema kuwa hawajui chanzo cha kukamatwa kwake, Kwani wamesema kikao hicho cha ndani kilifanyika kwa kufuata taratibu.