Michezo
Arsene Wenger apata wakati mgumu kumzuia Sanchez kuondoka
Kocha wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger huenda akawa na wakati mgumu wa kumshawishi mshambuliaji wake Alexis Sanchez kuendelea kubaki ndani ya timu hiyo.
Imedaiwa kuwa mshambuliaji huyo wiki hii amepokea ofa kutoka kwenye timu moja inayoshiriki ligi kuu ya China ikitaka kumlipa mshahara wa paundi 400,000 kwa wiki.
Kwa sasa Sanchez anayemaliza mkataba wake wa kuichezea timu hiyo mwaka 2018 anapokea mshahara wa paundi 130,000 kwa wiki.