Burudani
Asia Idarous kuiwakilisha Tanzania kwenye ‘The African Trader Show’ Marekani
Mbunifu mkongwe wa mavazi hapa nchini, Asia Idarous anatarajiwa kuiwakilisha Tanzania kwenye tamasha la mitindo la ‘The African Trader Show’ litakalofanyika nchini Marekani.
Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika kwa siku tatu kuanzia Septemba 2 hadi 4 mwaka huu huko California. Asia ni muasisi matamasha wawili ambayo ni ‘Kanga Za Kale’ na ‘ ‘Lady in Red’’.
Aidha mwandishi wa vitabu mkongwe hapa nchini, Yasin Kapuya na yeye amealikwa kwenye onesho hilo kama mtoa mada lakini pia ataonyesha kazi zake alizowahi kuzifanya.