Burudani

Barakah The Prince alia kufanyiwa hujuma akose views YouTube

Msanii wa muziki wa Bongo Flava, Barakah The Prince amedai kuwa YouTube account yake inafanyiwa mchezo mchafu ili ishusha idadi ya views.

Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Sometimes’ ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa views za ngoma yake hiyo zimekuwa zikishuka na kupanda na hata muda mwingine comment kufutwa.

“Kwa upande wa YouTube kuna mchezo mchafu unafanyika kwa sasa hivi, kwa mfano wimbo wangu kama jana ulikuwa ni namba saba kwenye trending ukiangalia video za watu wengine ni namba 40 lakini views wake ni milioni 4.4, nyingine inasoma namba 10 ukiangalia views zake ni laki 5.8 lakini mimi ambayo nina views elfu 20 ninasoma namba saba kwa nini iwe hivyo?” alihoji.

“Kuna mchezo mchafu unafanyika wa ku-block views wangu hata Mx kaniambia kuna mchezo mchafu unafanyika” ameongeza.

Amesema kuwa kuna baadhi ya nchini ikiwemo China mashabiki wake wamekuwa wakilalamika haiwapati video yake lakini video za wa wasanii wengine zinapatikana.

Hata hivyo ameweka wazi kuwa watu wenye access ya kuendesha account yake hiyo ni Mx Carter na Seven Mosha wa RockStar4000 kutokana na makubaliano ya hapo awali, pia ameeleza kuwa yupo katika utaratibu wa kufuta account hiyo na kufungua nyingine.

Ngoma ya Barakah ‘Sometimes’ video yake ilitoka October 28 mwaka huu lakini hivi sasa haipatikani YouTube (imeondolewa).

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents