Burudani

BBA The Chase: Penzi la Feza Kessy na Oneal lazidi kushamiri

Kama ulikuwa unahisi kuwa uhusiano wa Feza na Oneal unaishiwa fleva, basi hauko sahihi. Wandani hawa wameendelea kuiimarisha ngome yao ya mahaba ili kamwe isije kushambuliwa na wameendelea kupanga mipango ya kuliendeleza penzi lao baada ya The Chase.

foolforlovebig_74d1aab9-1a24-4e1d-bbad-f477f8add475_131323191318196

“We’re getting more serious,” Feza alimwambia Big Brother. “Kukutana na Oneal kwenye nyumba hii kumeonesha upande wangu ambao sikudhani watu wangeuona, alisema Feza. Upande wa ulaini na udhaifu wangu. Marafiki zangu nyumbani wanasema nimekuwa rahisi sana na napotea. Mtu mmoja anahitaji kwa kiasi fulani kuwa mjinga kwenye uhusiano.

Ni ngumu sana pia, sababu wakati mwingine nataka kuwa mkali na siwezi sababu uhusiano huu si tu unanihusu mimi. Unanihusu mimi Oneal na Africa.”

Feza alimwambia Biggie kuwa yeye na mpenzi wake huyo raia wa Botswana wana hamu kubwa siku wanaondoka mjengoni humo kwenda kuundeleza zaidi uhusiano wao.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents