Burudani

Blac Chyna kumpeleka Rob Kardashian mahakamani

Mwanamitindo na mfanyabiashara Angela Renee White a.k.a Blac Chyna, amemfungulia mashtaka mpenzi wake Rob Kardashian.


Blac na Rob enzi za mapenzi yao

Blac Chyna ambaye amezaa mtoto mmoja na Rob, wiki hii amejikuta akipokea mvua ya matusi na udhalilishaji pamoja na picha zake za utupu alizokuwa akimtumia mpenzi wake kuwekwa hadharani katika mtandao wa Instagram na mwanaume, ambaye anamtuhumu mpenzi wake huyo kuwamsaliti kwa kuwa na wanaume wengine kuwa mtumiaji wa madawa ya kulevya.

Mwanasheria wa mrembo huyo, Lisa Bloom ametumia ukurasa wake wa twitter, kutweet kwa kumjulisha Rob kuwa anatakiwa kufika mahakamani jumatatu kujibu tuhuma zinazomkabili za kumdhalilisha mpenzi wake huyo wa zamani.

“I represent Blac Chyna. I just gave Rob Kardashian notice that we’ll be in court Monday seeking restraining orders against him. More to come,” ameandika mwanasheria wa Blac.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents