Burudani

Cpwaa kuwarusha fainali za Big Brother

cpwaaa

Msanii Khalfan Ilunga ambaye anajulikana zaidi kama Cpwaa amefanikiwa kuwa msanii wa kwanza wa kitanzania kupata nafasi ya kupiga shoo katika fainali ya Big Brother Amplified 2011.     Msanii huyo Cpwaa anatarajiwa kupiga shoo katika fainali hizo pamoja na waimbaji wengine maarufu wa kitanzania ambao,

 

nipamoja na Fally Ipupa (DRC-Congo),wizkid na Mo Cheddah (Nigeria),Professor na Speedy wa AfrikaKusini.

katika taarifa kwa vyombo vya habari waandaaji wamesema show hiyo ya fainali ya Big Brother Amplified 2011 ambayo imejizolea umaarufu mkubwa pamoja na sherehe ya fainali ambapo mshindi atajinyakulia kiasi cha dola za kimarekani laki mbili pia itawajumuisha wasanii hao sita wa kiafrika pamoja na washiriki  wote waliotoka mapema.

katika taarifa hiyo kwa vyombo vya habari mkurugenzi wa Mnet Africa bwana Biola Alabiamesema “tutawapagawisha mashabiki wa shindano hili kwa kuwashtua na zawadi kubwa kabisa ambayo haijawahi kutokea katika shindano hili.

Najua mashabiki mtakuwa mnafahamu hivyo lakini washiriki waliomo ndani ya jumba la BBA Amplified hawajui kama kutakuwa na zawadi mbili za dola laki mbilimbili hivyo inatarajiwa kuleta mshtuko na hamasa kwa washiriki na watazamaji.

wakati huo huo shindano la mwaka huu la Big Brother Amplified 2011 limevunja rekodi ya wingi wa meseji kwa kupata jumla ya kura milioni 1 na laki 4 kwa wiki ya jana tu hivyo kufanya jumla ya idadi ya kura zote zilizopigwa kufikia milioni 6 na laki 3 na kuwa idadi kubwa zaidi ya kura katika mashindano yote ya Big Brother yaliyopita hivyo waandaaji wamewataka wapenzi wa shindano hilo kuendelea kupiga kura kwa wingi katika siku chache zilizosalia.

 

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents