Dani Alves: Kinacho wanyima mafanikio Arsenal ni wachezaji makinda na hivyo kukosa wazoefu
Beki Dani Alves wa Barcelona, Kuelekea mechi yao ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 bora, amesema wapinzani wao Arsenal wanakosa uzoefu ndiyo maana wanashindwa kupata mafanikio na kushinda mataji kwa wingi.
Kikosi hicho cha Arsene Wenger kitakuwa mwenyeji wa Barcelona katika mechi ya kwanza ya mtoano ya Ligi ya Mabingwa Jumanne usiku, na kauli hiyo ya Alves. Alizungumza na gazeti la The Times, Alves alisema kikosi hicho cha Wenger kimejaa wachezaji chipukizi na hivyo kukosa wazoefu ambao ni muhimu ili kupata mafanikio.
“Katika Premier League wanaanza vizuri, lakini wanashindwa kubaki katika ‘levo’ hiyo na kutwaa mataji. Wanacheza mpira vizuri sana na wamejipanga vizuri kimbinu, lakini hakuna mchanganyiko wa vijana na wazoefu. Vijana wanataka kushambulia, lakini kuna wakati unatakiwa kuwa na uwezo wa kumiliki mchezo,” alisema Alves.