Burudani
David Beckham akanusha uvumi kuwa ana mpango wa kuigiza kama James Bond
Mwakilishi wa mchezaji mstaafu wa soka wa Uingereza, David Beckham ameiambia Daily Mail kuwa staa huyo hana mpango wowote wa kuigiza kama James Bond.
Winga huyo wa zamani wa Manchester United amekanusha ripoti zilizosambaa kuwa ana mpango wa kugombea nafasi ya kuigiza kama James Bond mwakani, licha ya kuwa mashabiki wamejaribu pia kumuomba afanye hivyo.
Pamoja na kutokuwa na mpango wa kuigiza kama James Bond, Beckham ambaye ni baba wa watoto wanne ataonekana kwenye filamu ya ‘Knights of the Roundtable: King Arthur’.