Bongo Movie
Filamu ya DNA, yamuumiza Tito kichwa
Mkali wa filamu nchini, Tito Charlos, amesema amejiandaa kufanya filamu nyingi katika mwaka huu wa 2011 ili kuinua kipaji chake ambacho anahisi kinazorota.
Akidadavua na Bongo5, alisema kwa sasa anatarajia kuimalizia filamu yake, ya DNA ambayo ataishirikisha familia yake, wakiwemo mkewe na mtoto wake, ingawa hakusita kuongeza kuna ‘Problem’ kidogo imechomoza, ambayo inamuumiza kichwa kiasi cha kutomalizia filamu hiyo.
Alimalizia kwa kusema sasa atan’garisha sura kwenye sinema ya GIBANDA, iliyoandalia Mikoa mitatu Dar es salaam Mwanza na Mbeye.