Bongo Movie
Abzout kutoka kiasili
Abzout, msanii wa ngoma za asili na filamu nchini amesema yupo mbioni kuachia albamu yake, ambayo itarudisha tumaini jipya kwa wapendzi wa ngoma za asili.
Akiongea na Bongo5 alisema amejipanga kufanya nyimbo nyingi za kiasili na baadaye kuja kutoa albamu. Aliongeza kwa kusema yupo katika mikakati ya mwisho ya kwenda mkoani Mbeya kwa ajili ya kumalizia baadhi ya sehemu za ngoma hizo pamoja na filamu.
Aliwataja baadhi ya wasanii watakaoshiriki filamu ya Gibanda kuwa Riyama, Mzee Magari, Tito Charlos na Jackline Kisaka.