Bongo Movie
Mfalme Sele na 20% ndani ya filamu
Wale wakali wa Mashairi na ujumbe mzito katika muziki wa kizazi kipya, Mfalme Selemen na Twenty Percent, wanatarajia kutoka katika filamu moja iendayo kwa jina la ‘Haki ipo wapi?’.
Waliiambia Bongo5, kwamba filamu hiyo, itakuwa ni muendelezo wa ile ya ‘Furaha ipo wapi?’ huku wakiahidi hii itakuwa na vikorombwezo zaidi.
Walisema pia dogo Neema, ambaye alitesa kwenye filamu ya kwanza, atakuwepo tena kuongeza ladha zaidi.