Burudani
Genevieve Nnaji kuja na ‘Road to Yesterday’ baada ya kuwa kimya kwa miaka miwili
Baada ya kuwa kimya kwa kipindi cha miaka miwili, muigizaji wa Nigeria, Genevieve Nnaji anatarajia kurudi tena kwenye filamu.
Staa huyo wa Nollywood anatarajia kuja na filamu ya kwanza aliyoitayarisha mwenyewe, ‘Road to Yesterday.’
Nnaji alisema huu ni muda muafaka kwa yeye kurejea tena lakini akihusika zaidi pia kwenye utayarishaji. Amesema filamu hiyo aliyoshirikiana kuiandaa na Africa Magic itazinduliwa November 18, 2015.