Michezo
Hamilton ashinda taji la tatu la mashindano ya United States Grand Prix
Dereva wa magari, Lewis Hamilton ameendelea kufanya vizuri na kung’ara zaidi msimu huu baada ya kutwaa taji katika michuano ya United States Grand Prix.
Hamilton ameshinda michuano hiyo ya dunia na kutwaa taji lake la tatu kwa msimu huu wa michuano ya Formula 1.
Hamilton ambaye ni dereva wa timu ya Mercedes, anakua Muingereza wa pili baada ya Sir Jackie Stewart, kutwaa mataji matatu katika mbio hizo za magari.
Dereva wa timu ya Ferrari, Sebastian Vettel, alimaliza katika nafasi ya tatu nyuma ya dereva Nico Rosberg dereva wa timu ya Mercedes.