Burudani

Hemedy PhD ajutia maisha yake ya zamani, Akiri kutembea na mademu watano kila siku

Msanii wa Bongo Fleva na Muigizaji wa Filamu nchini Tanzania, Hemedy PhD amekiri wazi kuwa mtindo wa maisha yake ya miaka ya nyuma kipindi anapata umaarufu yalikuwa ni mabaya kitabia hususani kwenye mahusiano huku akidai kuwa alikuwa anapenda sana mademu.

Hemedy PhD

Hemedy amesema maisha hayo anayajutia hadi leo na amewaasa vijana wenzake kuwa wasiige mtindo huo wa maisha .

Mshindi huyo wa Shindano la Tusker Project Fame amedai kuwa kipindi cha nyuma alikuwa anatembea na wasichana hadi watano kwa siku.

Sio kitu cha kujivunia kwa sasa hivi ila ni maisha ambayo nimeyapitia na nisingependa viwana wengi ambao wanaonisikiliza sasa hivi wafanye hivyo, Lakini mzee mimi nilikuwa nakula mpaka mashine (Wanawake) watano kwa siku.“amesema Hemedy PhD kwenye kipindi cha Playlist cha Times FM huku akieleza kuwa muda mwingine alikuwa anapangisha Hotel kwa ajili ya kazi hiyo tuu

Ilikuwa ni panga pangua, Sometimes kabisa najenga kambi Hoteli mzee mimi nafumua tuu” amesema Hemedy PhD .

Hata hivyo Hemedy PhD amesema kuwa mpaka sasa hakumbuki ni mademu wangapi alitembea nao ila anachokumbuka ni kuwa ametembea mademu wengi kipindi cha nyuma alivyoanza kupata umaarufu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents