Unapoona Mtanzania mwenzako anafanya kitu kizuri, inapendeza na inatia moyo iwapo utatumia fulsa hiyo kumpa Big Up, tangu taaluma ya uzalishaji wa muziki iaminike imeshikiliwa na vinara kama vile Master Jay, Boni Luv, P-Funk, Mika Mwamba na wakongwe wengine, this time wametoa nafasi kwa vijana wanaochipukia
Unapoona Mtanzania mwenzako anafanya kitu kizuri, inapendeza na inatia moyo iwapo utatumia fulsa hiyo kumpa Big Up, tangu taaluma ya uzalishaji wa muziki iaminike imeshikiliwa na vinara kama vile Master Jay, Boni Luv, P-Funk, Mika Mwamba na wakongwe wengine, this time wametoa nafasi kwa vijana wanaochipukia na moja ya vijana hao ni Kijana Hermy B ambaye ujio wake kwa kweli unatishia amani katika upande wa uzalishaji wa Muziki.
Hermy B si jina geni katika gemu la muziki huu wa kizazi kipya kwani mchizi alianza kufanya shughuli za kuzalisha mabiti ya hatari kinyemela alipokuwa akifanya kazi katika kituo maarufu jijini cha redio Magic FM na hivi sasa amejikita rasmi kwa kuziachia kazi zake ambazo zimekuwa zikisikika na kukubalika ile mbaya kwani ameshafanya mikono kadhaa ambayo imebamba kama vile Kina kirefu ya Mansu-Li, Pwa (rmx) ya Cp, Binamu ya Mwanafalsafah na mikono kibao ambayo iko njiani inakuja.
Kwa kifupi mchizi anaweza na anastahili Big-Up za ukweli kabisa.