Michezo
Idris Sultan ampigia debe Samatta ligi kuu England na ligi kuu Uhispania Laliga
Idris Sultan ampigia debe Samatta ligi kuu England na ligi kuu Uhispania Laliga
Mshindi wa Big Brother Africa 2014 pia muigizaji na mchekeshaji kutoka Tanzania Idris Sultan ameonyesha mapenzi yake pia uzalendo kwa Mtanzania anayekipiga katika ligi kuu nchini Ubelgji Mbwana Samatta.
Idris ameonyesha mapenzi hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kunadi kuwa kila njia ifanyike ili mchezaji huyu akacheze ligi kubwa barani Ulaya kama ligi kuu nchini Uingereza na ligi kuu nchini Uhispania Laliga.
Mchekeshaji huyo ameamua kufunguka hayo kutokana na kiwango anachoendelea kukionyesha mchezaji huyo katika kilabu yake anayoichezea ya K.R.C Genk kwani ameisaidi kufuzu katika michuano ya UEFA Europa League 2018/19 kwa kufunga magoli matatu yaani hat-trick,lakini pia jana akifunga goli lingine.
Na huu ndio ujumbe wa Idris:-
Kijana sa hiv anajitahidi karudi kwny form