Burudani
Kenny Rogers atangaza kustaafu muziki
Mwimbaji mkongwe wa muziki wa Country, Kenneth Ray Rogers anayefahamika zaidi kwa jina la jukwaani kama Kenny Rogers, amesema kuwa baadaa ya ziara yake ya dunia anayotarajia kuifanya hivi karibuni atastaafu muziki.
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 77, ameyasema hayo Ijumaa ya Sept.25 katika kipindi cha ‘Today’.
Rogers ameongeza kuwa ziara hiyo aliyoipa jina la “Once Again Its Christmas Tour” itakayoanza Novemba 11,2015 ndio itakuwa ya mwisho ya kuwaaga mashabiki wake baada ya kuutumikia muziki kwa miaka mingi.
“Nahitaji kukaa na watoto wangu na mke wangu” alimalizia Rogers mwenye watoto watano aliowapata kutoka kwa wake zake wanne aliowahi kuwa nao.