Klitschko kuzichapa na Anthony Joshua
Hatimaye bondia wa Uingereza Anthony Joshua na bondia wa Ukraine Wladmir Klitschko wamekubali kuzichapa huku tangazo la pigano hilo likitarajiwa kufanywa katika siku za hivi karibuni, kulingana na promota Eddie Hearn.
Pambano hilo la uzani mzito linafaa kuidhinishwa na mkatanda wa Joshua wa IBF mbali na mikanda ya WBA na WBO.
Anthony Joshua
Bingwa wa ndondi katika uzani mzito duniani Tyson Fury alisalimu mataji yake ya WBO na WBA huku leseni yake ya kupigana ikifutiliwa mbali kwa muda.
Hata ivyo bodi ya Uingereza inayodhibiti leseni za mabondia ilimpokonya bondia huyo leseni yake kufuatia uchunguzi wa kutumia dawa za kusisimua misuli,baada ya bondia huyo mwenye umri wa miaka 28 kukiri kwamba amekuwa akitumia Cocaine ili kukabiliana na msongo wa mawazo.
Source: BBC