Burudani

Kumbe The Weeknd ndiye aliyempiga chini Selena Gomez!

Wadakuzi wa habari za kunyapia nyapia wameinasha ripoti kuwa muimbaji Abel Makkonen Tesfaye maarufu kama The Weeknd ndiye anza kumpiga chini mpenzi wake, Selena Gomez na sio kama inavyodaiwa na watu wengine.

Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, wameripoti kuwa mauhusiano ya wawili hao yaliingia dosari majira ya kiangazi na sio hivi karibuni kama vyombo vingi vinavyodai.

Licha ya mrembo huyo kuonekana na Justin Bieber hivi karibuni, ila inaelezwa kuwa Delena na The Weeknd bado ni washikaji na wanazungumza mara kadhaa.

Vile vile The Weeknd ameonekana siku chache byuma akifurahia maisha yake mapya bila mahusiano katika moja ya klabu ya mzuki huku akiwa na mrembo mwingine.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents