Burudani

Kylie aopoa rapa mpya baada ya Tyga

Zikiwa zimepita takribani siku kadhaa kwa msanii Tyga kuonekana na mrembo mpya, ambaye anadhaniwa ndio mpenzi wake wa sasa, wawili hao walionekana katika mitaa ya Los Angles kwenye mgahawa wa Serafina Sunset nchini Marekani.

Hatimaye naye ex wa rapa huyu, Kylie Jenner, naye ameamua kujiweka karibu na rappa Travis Scott. Picha za Kylie na Travis zilipigwa zikionyesha ukaribu waliokuwa nao wawili hao, hali iiliyoashiria huenda nao wako kwenye mahusiano.

Ingawa Kylie alikuja mwenyewe kutazama mchezo wa NBA uliokuwa ukiendelea mjini Houston, wadakuzi wa mambo walishuhusdia wawili hao wakishikana mikono kana kwamba ni wapenzi.

Huenda ikawa ni wakati mgumu kwa Kylie kuwa karibu na Travis Kwasababu, ameachana hivi karibuni na Tyga, na rapa Travis anatarajia kuondoka kuenda kwenye tour na Kendrick Lamar. Kama wasemavyo wadau wa masuala ya mahusiano, njia rahisi ya kumsahau mpenzi wako wa zamani ni kuwa na mpenzi mpya, na ndo walivyofanya Tyga na Kylie.

Na Laila Sued.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents