Burudani

Lady Jay Dee atoa jibu hili baada ya kushauriwa na shabiki avae madela kwenye video zake

Weekend hii Lady Jay Dee aliungana na wasanii wenzake wanaowania Tuzo za EATV kufichua siri ya mafanikio yao mbele ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Kampasi ya Mlimani), huku wakiwataka wanafunzi hao kuuliza baadhi ya maswali.

lady-jay

Moja kati ya swali ambalo aliulizwa muimbaji huyo na mmoja kati ya wanafunzi wao, kwanini anavaa nguo zisizo na maadili kwenye video zake wakati wanaweza kuvaa nguo za madela ambazo amedai ni za heshima.

Katika kujibu swali hiyo, Lady Jay Dee alisema yeye binafsi  hawezi kuvaa madela na ni nguo ambayo haipendi kuvaa.

“Mimi sipendi kuvaa madela kwa hiyo siwezi kuvaa dela kwenye wimbo wangu,” alisema Lady Jay Dee “Na mimi naamini sanaa unafanya kile kitu ambacho uko huru nacho na unakifanya kutoka moyoni,”

Pia muimbaji huyo amesema yeye anaamini mashabiki wake wanampenda vile anavyofanya ndio maana mpaka sasa anaendelea kufanya vizuri kwenye muziki wake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents