Burudani

Mabeste: Mimi si Rapper tu ninaweza kufanya kila kitu ndani ya muziki. Azungumzia sababu za kubadilika katika single yake mpya ‘Headache’

Wiki hii tumepokea wimbo mpya wa Mabeste uitwao ‘Headache’, wimbo ambao ameonesha kipaji chake kingine cha kuproduce, sababu ameproduce mwenyewe mdundo. Ukiusikiliza utagundua uko tofauti na nyimbo zake zilizopita kama Dole, Sirudi tena na Baadae ambazo ni Hip Hop.

mabeste

Wimbo mpya wa Mabeste ni club banger ambayo ameimba zaidi na ina mdundo ambao ukikutana nao club hautasita kusimama kutokana na unavyohamasisha kucheza.

Mabeste amesema kuamua kwake kubadilika kutoka style yake si kwa sababu za kibiashara lakini anapenda kufuata hisia zake zinavyomtuma.

“mimi si rapper tu peke yake ninaweza kufanya kila kitu ndani ya muziki, kwahiyo siwezi kuzuia hisia zangu ndani ya muziki endapo ninaona ninaweza kufanya.” Alisema Mabeste kupitia Planet Bongo ya East Africa Radio.

Akiongelea wasanii wa Hip Hop ambao huwa wanawachukulia tofauti rappers ambao huwa wanaamua kubadilika na kufanya aina tofauti ya muziki tofauti na Hip Hop amesema:

“Kwa artist ambaye anamchukia artist mwenzie ambaye amebadilika na kufanya kitu kingine ambacho ni kizuri pia ni ufupi wa akili tu, kwasababu kikubwa zaidi unachotakikana kufanya ni perferct , kitu ambacho kiko sahihi, ukishakuwa mwanamuziki huna tabaka la muziki unaweza ukafanya muzki wowote ilimradi ufanye vizuri, ukiuharibu ndio unakuwa umebugi.” Alimaliza Mabeste.

Isikilize hapa ‘Headache’

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents