Habari

Magazeti ya kibongo yaingizwa ‘mkenge’ na habari ya Mike Tyson kuwa mwanamke, habari ni ya uongo 100%

Vyombo vya habari nchini hususan magazeti leo vimeamka na vichwa vya habari kuhusiana na taarifa iliyoenea mtandaoni kuwa bingwa wa zamani wa ndondi duniani Mike Tyson amefanyiwa upasuaji na kubadilisha jinsia yake kuwa mwanamke.

Magazeti yalioandika habari hiyo ni pamoja na Mwananchi ‘Tyson adaiwa kubadili jinsi’, gazeti la Jambo Leo ‘Tyson awa Mwanamke’ na vyombo vingine.

Kwa kujiamini tunasema magazeti hayo yameingia ‘chaka mbaya’. Habari hiyo imeandikwa na mtandao wa http://www.newsbiscuit.com/ ambao asilimia 100 ya habari zake ni za kutunga.

Habari hiyo inasema Mike Tyson sasa ataitwa Michelle baada ya kufanyiwa upasuaji katika hospitali moja ya huko Beverley Hills nchini Marekani . Habari hii imeripotiwa na mitandao tofauti tofauti, pia gazeti la The Standard.
Habari hiyo inasema vyombo mbalimbali vya habari vimemnukuu akisema itakuwa amekamilisha ndoto yake pale atakapoanza kuona siku zake (hedhi), na kusema kuwa ili kukamilisha dhamira yake ya kuwa mwanamke’ jina lake ataitwa Michelle.

Kuna mambo mengi yanayoifanya habari hii iwe na walakini na kutufanya moja kwa moja tuamini kuwa si ya kweli. Kwa asilimia nyingi hii ni ‘hoax’ (a deliberately fabricated falsehood made to masquerade as truth.) Yaani ni habari ya ya uongo ama iliyotengenezwa ili kuifanya ionekane kama ya kweli.

Hizi ni sababu kubwa za kwanii hii ni habari ya uongo:

1. Habari hii inaonekana kutoka kwenye chanzo kimoja (newsbiscuits) na vyombo vingine vimekuwa vikiichukua kama ilivyo, neno kwa neno. Habari yenyewe ni hii:

America — Former undisputed heavyweight boxing champion of the world Mike Tyson is said to be “feeling fine” after undergoing successful gender reassignment surgery at a clinic near Beverley Hills.

Once known as “The Baddest Man on the Planet”, the boxer said having his first menstrual cycle “would be a dream come true”, and that from now on he would be known as Michelle.

“Some people might think it strange that I’m now a woman,” said Tyson, who underwent complete facial feminisation, orbital bone contouring and nasal surgery in an operation lasting over 16 hours.

‘But even at the height of my career, when pound for pound I was regarded as the best fighter in the world, I never lost touch with my feminine side and knew that one day I would grow breasts and have a vagina.’

Iron Mike was given the all-clear for gender reassignment surgery following a successful course in hormone replacement therapy which, in his autobiography, the boxer blamed for his 1996 defeat at the hands of Evander Holyfield.

Although at the time Tyson insisted he was fit enough to carry on with the fight, referee Mitch Halpern stopped the bout in the 11th round saying Tyson looked flushed, was sweating profusely and appeared to be lactating heavily from his left breast.

Tyson, said he hoped being female would finally convince the American people that his “bad-boy” days were over and he had turned over a new leaf.

2. Vyombo vinavyoheshimika kwa kuandika udaku duniani havijaandika habari hii.Kama ingekuwa kweli, hii ni habari kubwa mno kuachwa kuandikwa na mitandao kama The Sun, TMZ, mediatakeout na mingine. Hii ingekuwa habari kubwa mno pengine kuzidi hata kesi ya kulawiti watoto iliyokuwa ikimkabili Michael Jackson.

Jaribu kugoogle jina Mike Tyson kwenye sehemu ya ‘news’ na uone ni vyombo gani vimeandika habari hii. Umaarufu wa Mike Tyson duniani ungeifanya habari hii kutoandikwa na vyombo vya habari vya udaku tu bali pia mashirika makubwa kama BBC, CNN, Al-Jazeera na mengine yangetengeneza makala ndefu zenye undani mkubwa wa habari hii.

3. Akaunti zake mitandao ya kijamii hazioneshi mashabiki wake kuichukulia maanani habari hii. Tunafahamu jinsi mitandao ya kijamii inavyowaunganisha mastaa na mashabiki wao. Nenda kwenye akaunti ya Twitter ya Mike Tyson na angalia kama kuna mashabiki wanaomuuliza Tyson juu ya ukweli wa habari hii, Hakuna. Sababu ni kuwa hakuna kitu kama hicho na wengi wao hawana muda wa kuifuatilia.

4. Mike hawezi kuchukua uamuzi wa fedheha kama huo. Mike ni kitambulisho cha ujasiri na uanaume wa shoka, sio rahisi kujigeuza kuwa mwanamke, I mean come on Tyson anaweza kujigeuza kuwa mwanamke kweli?

Kwa asilimia 100 hii ni habari ya kutunga na ya uongo kama zile habari za wasanii kudaiwa kufa kwenye ajali. Bila utafiti hakuna haki ya kuongea.

Habari zingine za uongo zilizoandikwa na mtandao huo ni pamoja na ‘Abramovich amtaja Abramovich kuwa kocha wa Chelsea’, ‘Ndoa ya kwanza ya jinsia moja ya Nick Clegg na David Cameron yafungwa’, ‘Hatimaye Mungu akubali kumsaidia Malkia’, ‘Mgogoro wa mashariki ya kati wasuluhishwa kwenye Twitter’ na zingine nyingi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents