Michezo

Mamadou Sakho kuondoka Liverpool huenda akajiunga na Olympique Marseille

Klabu ya Olympique Marseille kutoka nchini Ufaransa, imeonyesha nia ya kumsajili beki wa kati wa majogoo wa jiji (Liverpool) Mamadou Sakho.

mamadou-sakho-559x520

Sakho ameshafunguliwa mlango wa kuondoka na kocha wa Liverpool Jurgen Klopp, kwa kuambiwa anaweza kuondoka wakati wa majira ya baridi (Mwezi Januari).

Olympique Marseille wanajiandaa kuwasilisha ofa ya usajili wa beki huyo mwenye umri wa miaka 26.

Mchezaji huyo alisajiliwa na Liverpool mwaka 2013 akitokea kwa mabingwa wa soka nchini Ufaransa Paris Saint-Germain.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents