Habari
Mgonjwa wa kwanza wa Corona apatikana Rwanda
Wizara ya Afya nchini Rwanda imethibitisha kuwepo kwa mgonjwa wa kwanza wa CoronaVirus nchini humo. Mgonjwa huyo ni raia wa India aliyefika nchini humo Machi 8. Siku ya jana Kenya nayo ilitangaza kumgundua mgonjwa wa kwanza hali ambayo ilizua taharuki zaidi kwa nchi za Afrika Mashariki kutokana na muingiliano wa watu.