Habari

Mr Nice kusaini mkataba na kampuni mpya Alhamis hii jijini Nairobi

Kwa mara nyingine tena, Mr Nice anatarajia kusaini mkataba mnono mbele ya waandishi wa habari jijini Nairobi, Kenya.

547548_532568053452436_1582451057_n

Nice atasaini mkataba mpya na ‘Candy n Candy Records’ Alhamis hii, July 25 kwenye kiota cha Lavish Lounge mida ya saa tano asubuhi.

Siku hiyo, Mr Nice ataongelea pia shutuma za ulevi, uzembe na uzinzi dhidi yake zilizodaiwa kuwa ni sababu za kupigwa chini na Grandpa Records.

Mr Nice alifukuzwa Grandpa Records huku baadhi ya mashabiki wakimcheka kuwa alienda Kenya kwa ndege lakini akaondoka kwa basi.

Source: Ghafla Kenya

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents