Michezo
Mshambuliaji Dimitar Berbatov apata mapokezi makubwa Ugiriki
Mshambuliaji Dimitar Berbatov aliyewahi kuvichezea vilabu vya Tottenham Hotspur, Manchester United,Fulham na AS Monaco amejiunga na klabu ya PAOK ya Ugiriki.
Dimitar Berbatov mwenye umri wa miaka 34 amejiunga na klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili akitokea katika klabu ya AS Monaco. Anakuwa mchezaji aliyeingia katika usajili wa kihistoria wa klabu ya PAOK.
Mchezaji huyo alitambulishwa mbele ya mashabiki 10000 katika uwanja wa Toumba ambao ni wengi kuwahi kutokea nchini humo hasa katika utambulisho wa mchezaji.