Nash MC awataka wasanii kupinga matumizi ya dawa za kulevya
Rapper Nash MC amewataka wasanii pamoja na wadau mbalimbali kupaza sauti zao katika kupinga matumizi ya dawa za kulevya.
Akizungumza kwenye kipindi cha Harakati cha Clouds TV kinachoendeshwa na Kalapina, Nash alisema kila mtu ana jukumu la kuelimisha vijana kuhusu matumizi ya dawa za kulevya.
Nash MC pamoja na Kalapina wakiwa katika harakati za kuelimisha jamii
“Baadhi ya wasanii wenzetu wengi wameingia huko, wengine wamefariki tumewazika, wengine marafiki zetu wa karibu tumewazika kitu ambacho kinauma kabisa,” alisema. “Hata jamii inafahamu kuna wasanii wenzetu wengi wamefariki kwa madawa ya kulevya. Mimi nimekuwa nikitumia muda mrefu kuongelea suala hili na kuwataka wasanii pamoja na wadau mbalimbali kuelimisha jamii juu ya athari za matumizi ya madawa ya kulevya.”
“Ndio maana pia nilimpigia Kalapina ili tuje tuzungumze na watu wa Temeke walioingia kwenye tatizo hili,” alisisitiza Nash.