Burudani

Nay wa Mitego: Tarajieni ngoma nyingine kubwa na Diamond

Nay wa Mitego amedai kuwa nyimbo za ushirikiano kati yake na Diamond hazijafika kikomo. Amedai kuwa wawili hao wanajiandaa kuja na ngoma nyingine – kubwa.

nay-wa-mitego-na-diamond-wakifanya-yao

“Kwa muda huu kidogo tunatoa gap, tutarudi na ngoma kubwa ya pamoja na tukiangalia mazingira ya album kuuzika basi tutaachia album ya pamoja mimi na Chibu,” Nay alimwambia mtangazaji wa kipindi cha SayariBit cha Pambazuko FM ya Ifakara, Morogoro, Keneth Ngamoga.

Nay alikuwa Ifarakara kwaajili ya show.

Kuhusu kutofanyika video ya wimbo wao Mapenzi au Pesa, Nay alisema ni kutokana na wote wawili kuwa na ratiba ngumu na zinazotofautiana.

Nay na Diamond walifanya vizuri na wimbo wao Muziki Gani.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents