Neymar na mchezaji mwenzake wa Barcelona wazichapa mazoezini (+Video)
Mshambuliaji wa Klabu ya Barcelona, Neymar Jr leo asubuhi amejikuta akitengeneza vichwa vya habari duniani baada ya kupigana na kinda wa Barcelona, Nelson Semedo wakiwa mazoezini nchini Marekani.
Kwa mujibu wa Gazeti la Marca taarifa zinasema Neymar alichezewa rafu na Nelson Semedo aliyesajiliwa msimu huu kutoka Benfica kitu ambacho alikichukulia kama amefanyiwa makusudi na ndipo akaanza kuvutana na kuanza kurushiana makonde.
Kwenye video iliyotolewa na mtandao wa Daily Mail inaonesha Neymar akionekana mwenye hasira kwani licha ya kuamuliwa na Javier Mascherano aliendelea kumfuata Nelson ili wazichape.
Hata hivyo ugomvi huo uliisha ingawaje Neymar alivua nguo za mazoezi na kurudi chumbani kwake huku akiwaacha wenzake wakifanya mazoezi.
Tayari kumeanza minong’ono kuwa kitendo hicho huenda kikawa kama chanzo cha yeye kuihama klabu hiyo baada ya tetesi za kuwindwa na matajiri wa ufaransa, PSG.