Habari
Ngoma ijayo ya Weusi inaitwa ‘Sweety Mangi’ washoot video yake SA
Ngoma mpya ya kundi la Weusi inaitwa Sweety Mangi, imefahamika.
Joh Makini, G-Nako na Nick wa Pili walikuwa jijini Johannesburg wiki hii kushoot video kadhaa ikiwemo ya wimbo huo.
Watatu hao wameshare picha kwenye kurasa zao za Instagram wakiwa location ya ndani kushoot video hiyo na muongozaji Justin Campos.
“Sweet mangi video….done….kaamkao wa kula,” ameandika Nick kwenye picha aliyoiweka Instagram.
Sweety Mangi si video pekee waliyoenda kushoot. Kabla ya hapo walishoot video nyingine ya wimbo wa Joh Makini aliomshirikisha staa wa Nigeria, Chidinma. Pia kuna wimbo waliomshirikisha rapper wa Afrika Kusini, Khuli Chana.