Burudani
Nina nyimbo za kufikisha album 13 – Barnaba
Msanii na mtayarishaji wa muziki wa High Table Sounds, Barnaba amedai kuwa kwenye store yake ya nyimbo ana albamu 13 na zote zina uzito usiobebeka ambao utakufanya utamani kusikiliza muda wote.
Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake wa ‘Lover Boy’ amesema hayo kupitia ujumbe aliouandika kwenye mtandao wa Instagram.
Kwenye Stock yangu nina Album kama 13 ivi kwa haraka haraka Na kila nikipekua naona chuma kimebebana na chuma lakini najaribu kuangalia Album yangu Ya 8/8 naona kama imezidi Vyuma Vyote na inaitaji Nafasi Ya masikio Ya wengi Sijui nipeleke sijui muda ndo bado Mana ilibidi Itoke tangu mwezi 8 tarehe 8 mwaka huu /na ina nyimbo 8 ambazo sidhani kama unaweza Peleka wimbo mbele …!!!????????????????????????