Burudani

Nyota wa Bollywood Sanjay Dutt atoka jela

Nyota wa filamu za Bollywood, Sanjay Dutt ameachiwa kutoka jela alipokuwa amefungwa katika mji wa magharibi wa Pune nchini India.

160224154131_sanjay_dutt_promotion_payroll_512x288_crispybollywood_nocredit

Dutt mwenye umri wa 56 alihukumiwa kifungo jela kufuatia makosa ya kumiliki silaha inayohusishwa na mlipuko wa 1993 mjini Mumbai ambapo takriban watu 257 waliuawa na wengine 713 kujeruhiwa.

Dutt alipatikana na hatia ya kununua silaha hiyo kutoka kwa walipuaji ,lakini yeye akasema kwamba silaha hiyo ilikuwa muhimu kwa lengo la kuilinda familia yake wakati wa ghasia za Waislamu dhidi ya Hindu.

Baadaye alipelekwa hadi jela ya Pune mwaka 2013 ili kukamilisha kipindi chake cha miaka mitano. Hata hivyo alipewa msahama wa siku 144 baada ya kuonekana kuwa na tabia njema na vitendo kama vile kusimamia kipindi cha redio.

Source: BBC

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents