One Africa: Enos Olik wa Kenya aongoza video ya Butera Knowles wa Rwanda aliyemshirikisha Roberto wa Zambia
Kiwanda cha muziki cha Afrika kinazidi kuungana pamoja.
Kuanzia Kushoto: Butera Knowles, Enos Olik na Roberto
Miaka ya hivi karibuni wasanii wa Afrika wamekuwa wakishirikiana kwenye nyimbo zao za hivyo kuzidi kuusogeza karibu zaidi muziki wa bara hili.
Baada ya kutoka kuongoza video ya wimbo wa Christian Bella na Alikiba ‘Nagharamia’ iliyofanyika nchini Afrika Kusini, Enos Olik ameongoza tena video ya collabo ya wasanii wa Afrika.
Butera na Roberto walipokuwa wakielekea Nairobi kushoot video ya wimbo wao Te Amo
Ni wimbo wa msanii wa Rwanda, Butera Knowles aliomshirikisha hitmaker wa ‘Amarula’ Roberto wa Zambia. Knowles ni msanii mkubwa wa Rwanda kama alivyo Vanessa Mdee kwa Tanzania.
Video hiyo inafanyika nchini Kenya.
“It’s all smiles with @buteraknowless and @robertozambia. When different cultures meet… #comingsoon,” aliandika Olik kwenye picha aliyoiweka Instagram.