Picha: NMB yafadhili semina ya maafisa maendeleo wa vijana nchini
Benki ya NMB imefadhili semina kubwa iliyohusisha maafisa maendeleo wa vijana kutoka nchi nzima.Semina hiyo ya siku mbili ilifanyika katika kumbi za uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Mhe. Dkt. Fenera Mukangara ambaye ni Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo akiongea na maafisa maendeleo ya vijana nchini wakati wa uzinduzi wa semina ya siku mbili
Mhe. Dkt.Fenera Mukangara ambae ni Waziri wa Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo alizindua rasmi semina hii na kuishukuru Benki ya NMB kwa ufadhili mkubwa ambao wamejitolea ili kufanikisha semina.
Katibu Mkuu Wizara ya Habari ,Vijana,Utamaduni na Michezo Bw. Seth Kamuhanda akifafanua jambo wakati wa semina hiyo.
Meneja wa NMB Mikopo Midogo Midogo Bw. Mashaga Changarawe akielezea huduma mbali mbali zitolewazo na Benki ya NMB zikiwemo akaunti pamoja na mikopo mbalimbali kwa wajasiliamali
Meneja Mawasiliano wa NMB, Josephine Kulwa akizungumzia jinsi ambavyo Benki ya NMB kwa kupitia huduma zake kwa wajasiliamali inavyosaidia kuongeza ajira kwa vijana nchini
Sehemu ya washiriki wa semina hiyo
Erick Shigongo nae alitoa maada kuhusiana mafanikio na kujitambua katika ajira
Dhumuni la semina ni kujadili maendeleo ya vijana kuanzia ngazi ya halmashauri,kuimarisha utendaji kazi kwa vijana wa mikoa na wilaya.