Habari
Rais Magufuli ajibu ombi la viongozi wa dini la kufungia kampuni za kubeti na kubashiri (+video)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa serikali itachunguza kwa ukaribu makampuni ya kubeti na kubashiri Tanzania, ili kuangalia namna ya kuilinda jamii kwani makampuni hayo yamekuwa yakitangazwa sana kwenye vyombo vya habari.
Ombi hilo la kuhusu kampuni za kubeti, limetolewa na Mzee Adam leo Januari 23, 2019 Ikulu wakati Rais Magufuli alivyokuwa akisikiliza changamoto mbalimbali za viongozi wa Dini nchini.