Uncategorized

Katika hali isiyotarajiwa Mbao FC yaifunga Gor Mahia na kuitoa nje ya michuano ya SportPesa miamba hiyo ya soka kutoka Kenya

Achana na habari za Mnyama Simba kufungwa bao 5 – 0 kutoka kwa AS Vita Club ya DR Congo au Bi Hindu kumfunda DiamondPlatnumz kuhusu kuoa. Kubwa kwenye mchezo wa soka hivi sasa ni michuano ya SportPesa inayoendelea uwanja wa taifa ambapo katika hali isiyo kuwa ya kawaida bingwa mtetezi timu ya Gor Mahia imeyaaga mashindano hayo baada ya kupokea kipigo kutoka kwa Mbao FC ya Tanzania.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida na wala isiyotarajiwa na wengi mabingwa watetezi Gor Mahia wameyaaga mashindano hayo kwa kutolewa na timu changa ya Mbao FC kupitia mikwaju ya penati.

Katika penati hizo Mbao FC imekosa moja kati ya tano ilizopiga wakati Gor Mahia wakikosa mbili kwenye mikwaju hiyo mitano.

Mpaka dakika 90 zinakamilika timu hizo zilitoka sare ya bao 1 – 1 ghali iliyopelekea kupigwa mikwaju ya penati ili kupata mshindi atakayesonga hatua inayofuata.

Bao la kuongoza la Gor Mahia likifungwa na Denis Oliech kupitia mkwaju wa penati baada ya Amos Charles kuunawa mpira ndani ya 18 katika haraka za kuokoa wakati Mbao FC wakipata goli la kusawazisha kupitia Aboubakar Ngalema. 

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents